• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 10:08 PM
SHAIRI: Ndoto yangu yazimika

SHAIRI: Ndoto yangu yazimika

Na Sylvester Kibet Kiplagat 

Msinidhulumu nina haki,

Msinidunishe kwa kuwa msichana,

Nina haki ya kupata elimu kama wengine,

Msinioze ningali mchanga kimawazo.

 

Niruhusu niboreshe maisha ya usoni,

Baba, mama, mbona mwautesa moyo wangu?

Mawazo yafifisha nafsi yangu,

Ndoto yangu mwaizima pole pole.

 

Kama upepo upumavyo kutoka kusini hadi kaskazini,

Ndivyo mwayapeperusha maisha yangu,

Niruhusu niboreshe maisha yangu,

Mila na desturi zilizopitwa na wakati zanizuia.

 

Masomo nipate, ulimwenguni nitambe,

Maisha yapate maana, heshima nipate,

Nijue kuandika, na kutangamana na wengine,

Nisipewe mkuki kwenda shida malishoni .

 

You can share this post!

SHAIRI: Ubakaji kama makaa

Jinsi ya kuandaa minofu ya kuku iliyopakwa siagi