NA GEOFFREY ANENE
BINGWA wa Jumuiya ya Madola na Afrika mbio za mita 100, Ferdinand Omanyala aliwapa raha mashabiki wake baada ya kuhifadhi taji lake kwenye Riadha za Absa Kip Keino Classic Continental Tour ugani Moi Kasarani mnamo Jumamosi.
Afisa huyo wa polisi amefyatuka umbali huo kwa sekunde 9.84.
Amewaonesha kivumbi Waamerika Kenny Bednarek (9.98) na Marvin Bracy (10.03).