• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 9:12 AM
Aubameyang aongoza Barcelona kuzamisha Bilbao katika La Liga

Aubameyang aongoza Barcelona kuzamisha Bilbao katika La Liga

Na MASHIRIKA

PIERRE-Emercik Aubameyang alifunga bao lake la tano kutokana na mechi tatu katika kikosi cha Barcelona na kuongoza waajiri wake wapya kukomoa Athletic Bilbao 4-0 katika mechi ya Ligi Kuu ya Uhispania (La Liga) mnamo Jumapili.

Mshambuliaji huyo wa zamani wa Arsenal aliwaweka Barcelona kifua mbele katika dakika ya 37 baada ya fataki ya Gerard Pique kugonga mwamba wa lango la Bilbao.

Ousmane Dembele alifunga bao la pili la Barcelona kabla yam engine kujazwa kimiani na Luuk de Jong na Memphis Depay.

Depay (mabao tisa) na De Jong (mabao sita) ndio wachezaji wengine wanaomzidi Aubameyang katika kufungia Barcelona magoli zaidi msimu huu licha ya kwamba nyota huyo raia wa Gabon alitua ugani Camp Nou mwanzoni mwa Februari 2022.

Barcelona hawajapoteza mechi yoyote chini ya dakika 90 tangu Disemba 8, 2022. Ushindi dhidi ya Bilbao uliwapaisha hadi nafasi ya nne kwenye msimamo wa jedwali la La Liga kwa alama 45 sawa na mabingwa watetezi Atletico Madrid wanaofunga orodha ya tano-bora.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Liverpool mabingwa wa Carabao Cup

Maonyesho ya kahawa yaliyoleta pamoja zaidi ya wakulima...

T L