• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Obiri kutetea taji la Great Manchester Run mnamo Mei 21

Obiri kutetea taji la Great Manchester Run mnamo Mei 21

Na GEOFFREY ANENE

MALKIA mpya wa Boston Marathon, Hellen Obiri atarejea nchini kutetea taji lake la mbio za kilomita 21 la Great Manchester Run hapo Mei 21.

Waandalizi wa mbio hizo wamethibitisha Mei 18 kuwa bingwa huyo wa zamani wa Afrika, Jumuiya ya Madola na dunia wa mbio za mita 5,000 atakuwa miongoni mwa majina makubwa yatakayoshiriki.

Obiri alitwaa taji la Great Manchester Run 2022 kwa dakika 30 na sekunde 15.

Ushindani mkubwa kwa Obiri anayeishi na kufanyia mazoezi yake nchini Amerika, unatarajiwa kutoka kwa bingwa wa Olimpiki mbio za marathon Peres Jepchirchir kutoka Kenya pamoja na Muethiopia Senbere Teferi.

Jepchirchir alimaliza London Marathon katika nafasi ya tatu mwezi uliopita wa Aprili.

Steph Twell ataongoza orodha ya washiriki wa kitengo cha kinadada kutoka Uingereza kwenye Great Manchester Run ambayo pia ina Mollie Williams, Monika Jackiewicz, Lily Partridge, Rose Harvey na Natasha Cockram. Mbio hizo zinatarajiwa kuwa za mwisho za mshindi wa 2018 Mo Farah.

  • Tags

You can share this post!

Wafukuaji wa maiti Shakahola wafunguka

‘Nabii’ kortini kwa madai ya kubaka binti 2 wa mshirika...

T L