• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
Diwani afariki baada ya vurugu kuzuka mkutanoni

Diwani afariki baada ya vurugu kuzuka mkutanoni

NA SHABAN MAKOKHA

DIWANI (MCA) wa Kisa Mashariki  Stephen Maloba amefariki dunia baada ya wahuni kumvamia na kumdunga kwenye farakano baina ya upande wake na wa mbunge wa Khwisero Christopher Aseka.

Polisi Kakamega wamethibitisha kifo cha MCA huyo.

“Nina habari za kifo cha diwani kilichotokea Khwisero lakini bado ninakusanya mengi kuhusu kilichotokea,” Kamanda wa Polisi Kaunti ya Kakamega Joseph Kigen amesema.

Gavana wa Kakamega Fernandes Barasa amelaani mauaji hayo lakini pia akawataka wakazi na wenyeji wa kaunti hiyo waishi kwa amani.

Seneta wa Kakamega Dkt Boni Khalwale ameandika kwenye ukurasa wake wa Twitter akithibitisha kifo cha Bw Maloba.

“Niko katika mochwari ya Hospitali ya Mbale nikishughulika baada ya diwani wa Kisa, Mheshimiwa Maloba kuuawa kwa kudungwa kwenye mzozo na Mheshimiwa Aseka ambaye ni Mbunge wa Khwisero,” ameandika Seneta Khalwale.

  • Tags

You can share this post!

STAA WA SPOTI: ‘Neymar’ wa Falling Waters ya Barcelona...

Wakazi 160,000 Tana River waumizwa na njaa

T L