Na WANDERI KAMAU
SUALA lililozua gumzo wiki hii ni majibizano yaliyozuka kati ya mrengo wa Naibu Rais William Ruto na mwanasiasa Maina Njenga (Laikipia), baada ya watu wanaodaiwa kuwa wafuasi wa Bw Njenga kumzomea vikali Dkt Ruto alipofanya kampeni katika eneobunge la Laikipia Magharibi, Kaunti ya Laikipia.
Kwa ghadhabu, Dkt Ruto aliwakosoa vikali watu hao, akiwaambia kuandaa mkutano wao badala ya kuvuruga mkutano wake.Ni hali iliyozua hisia kali kati ya Bw Njenga (anayelenga kuwania Useneta katika kaunti hiyo) na washirika wa Dkt Ruto, hasa mbunge Aden Duale (Garissa Mjini).