Na KNA
NAIBU Gavana wa Kaunti ya Busia, Bw Moses Mulomi (Pichani), ametangaza azma yake ya kugombea ugavana kumrithi Gavana Sospeter Ojaamong.
Bw Mulomi alisema anafaa kwa wadhifa huo na kupuuza wagombeaji wengine kama wasiojali maslahi ya wakazi wa Busia.
Alisema hayo alipohudhuria mazishi eneo la Butula.