• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 9:50 AM
Raila aongeza kasi ya maandamano jijini

Raila aongeza kasi ya maandamano jijini

NA MWANDISHI WETU

KIONGOZI wa Azimio La Umoja-One Kenya amesema ni muhimu Katiba ifanyiwe marekebisho ili mbunge anayenunuliwa aende nyumbani.

Akiongea katika eneo la Mukuru Kwa Njenga, Raila amesema inasikitisha kwamba baadhi ya wabunge wa Azimio walinunuliwa na serikali ya Rais William Ruto kama njia mojawapo ya kuhujumu upinzani.

“Katiba ifanyiwe marekebisho mbunge anayenunuliwa arudi kwa wananchi kuomba kura upya,” amesema Raila.

Awali pia amesema wananchi wanapitia hali ngumu sana kiuchumi na kusisitiza ni sharti serikali iteremshe bei za bidhaa na ada za huduma muhimu kama umeme.

“Tunasema ni lazima bei ya unga irudi chini, serikali iteremshe bei ya stima, na server ya IEBC ifunguliwe,” amesema kiongozi huyo wa Azimio.

Viongozi wengine kwenye msafara huo wa maandamano ni Martha Karua, Eugene Wamalwa, Mbunge wa Embakasi Mashariki Babu Owino, Prof George Wajackoya miongoni mwa viongozi wengine.

  • Tags

You can share this post!

12 wafariki kwenye ajali Naivasha

Raila alaani uvamizi katika shamba la Uhuru Ruiru

T L