Simanzi kuu kufuatia kifo cha aliyekuwa mwandishi wa ‘Taifa Leo’

Simanzi kuu kufuatia kifo cha aliyekuwa mwandishi wa ‘Taifa Leo’

Na Charles Wanyoro

SIMANZI imegubika jumuiya ya waandishi baada ya mmoja wao kutoka Meru, Bw Darlington Manyara, 29, kuaga dunia Jumanne.

Iliripotiwa kuwa Bw Manyara alifariki baada ya kuwa mgonjwa kwa kipindi kifupi. Alikuwa anapata matibabu katika hospitali ya Meru Level 5.

Bw Manyara aliwahi kufanya kazi katika kampuni ya kusambaza habari ya Nation Media kabla ya kuhamia Standard Media Group.

“Bw Manyara alikuwa mwandishi shupavu na ustadi wake ulionekana pale alipochambua siasa za Meru,” alisema Wainaina Ndung’u ambaye walifanya kazi pamoja.

Familia, jamaa, marafiki na waandishi wenzake walimtaja marehemu kama mwenye bidii na kupenda kutangamana na watu.

“Katika uandishi wake, aligusia siasa, uhalifu, korti na hata kilimo. Alijua kuunda uhusiano mzuri na wadokezi wake na hata marafiki,” akasema Bw Ndung’u.

Mwili wa marehemu ulipelekwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha hospitali ya Meru Level 5.

 

You can share this post!

Mawakili waapa kumkabili Joho

JSC yakutana kusaka mrithi wa Maraga

adminleo