• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 5:54 PM
Clarke Oduor asuka pasi kusaidia Barnsley kuokota alama dhidi ya Birmingham ligini

Clarke Oduor asuka pasi kusaidia Barnsley kuokota alama dhidi ya Birmingham ligini

Na GEOFFREY ANENE

BEKI Mkenya Clarke Oduor anaendelea kung’ara kambini mwa Barnsley baada ya kusaidia klabu hiyo ya Ligi ya Daraja la Pili nchini Uingereza kutoka 1-1 dhidi ya Birmingham ugani Oakley mnamo Agosti 28.

Oduor hakutumiwa na Valerien Ismael katika michuano 27 ya mwisho ya ligi ya msimu 2020-2021 na aliaminika atahamia kwingineko kabla ya kocha huyo Mfaransa kunyakuliwa na West Bromwich Albion.

Kocha mpya Markus Schopp kutoka Austria amekuwa akimpa Oduor nafasi zaidi na hajajutia kufanya hivyo.

Katika michuano mitano ya ligi hiyo msimu huu wa 2021-2022, Oduor amecheza dakika 380 ikiwemo 90 dhidi ya Birmingham.

Clarke Oduor. Picha/ Hisani

Pia, alicheza mechi nzima katika Kombe la Carabao dhidi ya Bolton Wanderers.

Hapo Agosti 28, Oduor,22, alisukia nahodha Callum Styles pasi iliyozalisha bao la mapema katika dakika ya sita. Oduor alisumbua wapinzani katika mchuano huo ambao Lukas Jutkiewicz alisawazisha dakika ya 33.

Birmingham ni nambari tano kwa alama nane nayo Barnsley inapatikana katika nafasi ya 14 kwa alama sita kwenye ligi hiyo ya timu 24 inayoongozwa na Fulham kwa alama 13.

You can share this post!

Mwanamume apatikana amefariki gesti

Jinsi ya kuandaa buns zenye ufuta