• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
Mwanamuziki Koffi Olomide ahukumiwa kwa kupatikana na hatia ya kuwazuilia wachezaji densi

Mwanamuziki Koffi Olomide ahukumiwa kwa kupatikana na hatia ya kuwazuilia wachezaji densi

Na PATRICK ILUNGA

KINSHASA, DRC

MWANAMUZIKI wa mtindo wa Rhumba, Koffi Olomide kutoka DRC Congo, amehukumiwa kifungo cha miezi 18 gerezani kwa kuteka nyara wachezaji densi wake wa zamani.

Hata hivyo, ni kifungo kinachompa fursa ya kujirekebisha tabia akiwa chini ya uangalizi.

Hukumu hiyo ilitolewa na mahakama moja mjini Versailles, Ufaransa, Jumanne.

Hata hivyo mwanamuziki huyo aliondolewa mashtaka ya dhuluma za ngono dhidi ya wachezaji densi hao waliokuwa wanachama wa bendi yake ya Quartier Latin.

Inadaiwa alitekeza vitendo hivyo kati ya mwaka wa 2002 na 2006 katika makazi yake yaliyo katika eneo la Asnières, viungani mwa jiji la Paris.

Mnamo 2019 alikabiliwa na shtaka la ubakaji dhidi ya msichana wa miaka 15.

Mara ya kwanza, mahakama ya Nanterre ilimpa kifungo cha nje cha miaka miwili badala ya kifungo cha miaka saba kama ulivyotaka upanda wa mashtaka.

Alipewa hukumu hiyo ijapokuwa hakuwepo mahakamani ilipotolewa.

Akijitetea, alisema lengo la wachezaji densi hao lilikuwa kumtumia kupata stakabadhi za kukaa na kufanya kazi nchini Ufaransa.

You can share this post!

Ghana kuwapiga faini wanaosafiri huko bila vyeti

Muungano wapendekeza adhabu kali kwa wazalishaji mbegu...

T L