• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
Lori la polisi lagonga nyumba za mtaa wa mabanda

Lori la polisi lagonga nyumba za mtaa wa mabanda

Na STEVE NJUGUNA

LORI la polisi Jumamosi lilikosa mwelekeo na kugonga nyumba za watu katika mtaa wa mabanda wa Maina, viungani mwa mji wa Nyahururu, Kaunti ya Laikipia.

Kwa mujibu wa Naibu Chifu Purity Mumbi, dereva wa lori hilo lililokuwa kwenye barabara ya Nyahururu-Maralal alipoteza udhibiti wake kisha likagonga nyumba hizo za mbao na kusababisha uharibifu mkubwa.

Hata hivyo, wananchi walifika katika eneo la tukio hilo baada ya ajali hiyo ya saa mbili usiku na kumwondoa mtoto mwenye umri wa miaka 10 ambaye alikuwa amefunikwa kwenye vifusi.

Mtoto huyo mvulana alivunjika mguu na akapelekwa hospitalini.

You can share this post!

Harambee Stars yarejea nyumbani na pointi moja kampeni ya...

Afueni kwa wakazi wa Gatuanyaga barabara ikianza kujengwa