• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 9:35 PM
Mamelodi anayochezea Mkenya Brian Mandela yapoteza ufalme wa Nedbank Cup

Mamelodi anayochezea Mkenya Brian Mandela yapoteza ufalme wa Nedbank Cup

Na GEOFFREY ANENE

MAMELODI Sundowns anayochezea Mkenya Brian Mandela Onyango ilivuliwa taji la Kombe la Nedbank, Jumapili.

Hii ni baada ya kulemewa katika upigaji wa penalti 6-5 dhidi ya Tshakhuma Tsha Madzivhandila (TTM) katika nusu-fainali mjini Pretoria.

Beki Onyango aliingia katika muda wa ziada katika dakika ya 103 kujaza nafasi ya Aubrey Modiba. Aliondosha hatari dakika tano baadaye kabla ya kupachika bao dakika ya 114. Hata hivyo, bao lake halikusimama kwa sababu alipatikana ameotea.

Lyle Lakay, Sibusiso “Vila” Vilakazi, Ricardo Nascimento, Thapelo Morena na Themba “Mshishi” Zwane walifunga penalti zao, lakini nahodha Hlompho Kekana akapoteza yake. Tshakhuma ilifunga zake zote na kujikatia tiketi ya fainali. TTM itamenyana na Chippa United katika fainali mnamo Mei 8. Chippa ililaza Pretoria Callies katika nusu-fainali ya kwanza mnamo Aprili 17.

You can share this post!

Kipa Courtois awaokoa Real Madrid dhidi ya Getafe kwenye...

Mfumo mbadala wasaidia KRA kukusanya Sh21 bilioni