• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 4:36 PM
Avokado husaidia hasa wanawake kuyeyusha mafuta tumboni – Utafiti

Avokado husaidia hasa wanawake kuyeyusha mafuta tumboni – Utafiti

Na Leonard Onyango

KULA parachichi (avocado) kila siku kunaweza saidia wanawake kupunguza mafuta tumboni, kulingana na utafiti uliofanywa nchini Amerika.

Watafiti wa Chuo Kikuu cha Illinois Urbana-Champaign walisema mafuta ya avokado husaidia katika kuyeyusha mafuta tumboni.

“Utafiti wetu umebaini kuwa mafuta kutoka avokado husaidia sana katika kupunguza mafuta tumboni,” ikasema ripoti ya utafiti huo.

Kulingana na watafiti hao, kuna aina mbili za mafuta tumboni mwa binadamu; mafuta ambayo huwa chini ya ngozi (subcutaneous fat), na mafuta ambayo hujilimbikiza ndani ya tumbo, inayojulikana kama mafuta ya utumbo (visceral).

Mafuta ya utumbo huzunguka viungo vya ndani kwenye tumbo.Watu walio na idadi kubwa ya mafuta mazito ya utumbo huwa katika hatari kubwa ya kupata ugonjwa wa kisukari.“Ukikula avokado, kuna uwezekano wa mafuta ya utumbo kuyeyuka haraka,” wakasema watafiti hao.

Wanawake walioshiriki utafiti huo waligawanywa katika makundi mawili; kundi la kwanza walikula avakado kila siku na jingine walikula chakula bila tunda hilo.

Baada ya wiki 12 walipimwa na kubainika kwamba waliokula avokado kila siku walikuwa na kiwango cha chini cha mafuta ikilinganishwa na wenzao.

 

You can share this post!

Congo yajifua kubaki ligini, Buruburu ikilia maamuzi ya...

Ukweli kuhusu chanjo za corona zilizoruhusiwa nchini