• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 9:50 AM
Casemiro abeba Manchester United dhidi ya Reading katika Kombe la FA

Casemiro abeba Manchester United dhidi ya Reading katika Kombe la FA

Na MASHIRIKA

KIUNGO Carlos Casemiro alidhihirisha jinsi alivyo nguzo kubwa kambini mwa Manchester United kwa kufunga mabao mawili katika ushindi wa 3-1 dhidi ya Reading katika Kombe la FA ugani Old Trafford.

Ushindi huo ulikatia Man-United tiketi ya raundi ya 16-bora na kuweka hai matumaini yao ya kutwaa Kombe la FA kwa mara ya 13 katika historia kadri wanavyofukuzia pia ubingwa wa EPL, Carabao Cup na Europa League muhula huu.

Kikosi hicho cha Erik ten Hag kwa sasa kinakamata nafasi ya nne kwenye jedwali la EPL kwa alama 39 sawa na nambari tatu Newcastle United ambao pia wamepiga mechi 20. Kitaalika Nottingham Forest kwa mkondo wa pili wa nusu-fainali ya Kombe la FA mnamo Februari 1 kabla ya kuendea Barcelona kwa mkondo wa kwanza wa hatua ya 16-bora ya Europa League wiki mbili baadaye.

Man-United walipata bao lao jingine dhidi ya Reading kupitia kwa Fred de Paula Santos, sekunde chache baada ya Andy Carroll kuonyeshwa kadi nyekundu katika kipindi cha pili. Miamba hao wa Uingereza walijizolea Kombe la FA mara ya mwisho mnamo 2016, baada ya kukomoa Crystal Palace 2-1 kwenye fainali ugani Wembley.

“Casemiro ni mchezaji wa haiba kubwa mwenye tajriba pevu. Huwezi ukashinda mataji anayojivunia kitaaluma bila kuwa na utajiri wa maarifa kame yake,” akasema nahodha wa Man-United, Harry Mguire.

“Amefanya kazi aliyoletwa kufanya aliposajiliwa Agosti 2022. Ni miongoni mwa wachezaji bora tunaojivunia kikosini kwa sasa. Anajua pa kusimama uwanjani na jinsi ya kukabili wapinzani,” akaongezea Ten Hag.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Son Heung-min asaidia Tottenham kuingia raundi ya 16-bora...

Chelsea wajinasia huduma za beki Malo Gusto kutoka...

T L