• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 4:10 PM
Huddah Monroe: Ndoa si ndoto yangu, kwa nini nijipe ‘stress’?

Huddah Monroe: Ndoa si ndoto yangu, kwa nini nijipe ‘stress’?

NA JOHN KIMWERE

MWANAMITINDO na mwanasosholaiti Huddah Monroe ameelezea haja ya wahusika kwenye ndoa kuficha maisha yao binafsi, akionya kinachochangia talaka na wapendanao kuachana ni ‘kujianika hadharani hasa mitandaoni’.

Msanii huyo hata hivyo amekiri kwamba ndoa si ndoto yake, kufuatia milima na mabonde inayopitiwa kwenye mahusiano.

Anashikilia kwamba ikiwa angepata nafasi kuingia katika ndoa angeificha sana kamwe asingependa iwe machoni mwa umma saana.

“Buda ndoa sio matembezi kwenye bustani,” akasema.

Huddah mwenye umri wa miaka 31, alisema hayo kupitia Instagram yake kipindi cha kujibu maswali ya mashabiki.

Alikuwa akijibu swali la; Ni kwa nini hajapata mwanaume wa kumuoa rasmi ilhali ni dada mwenye urembo wa kuvutia. Akiendelea kumjibu mfuasi huyo, alimuuliza ikiwa amewahi kujiuliza kwa nini ndoa si ndoto ya kila mmoja?

“Jameni, ndoa si mteremko kama mnavyofikiria. Ina changamoto kibao ambazo baadhi yetu hatuwezi kustahimili,” akasema.

Huddah ambaye wakati mwingine anaishi Dubai kwa muda mrefu, amekuwa msiri sana kupita maji kuhusu mahusiano yake.

Itakumbukwa kuwa 2022 alidaiwa kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na mwanamuziki wa Bongo, Juma Jux baada ya wawili hao kuonekana pamoja mara kadhaa hadharani.

Wawili hao walionekana pamoja wakifanya mambo mbalimbali, ikiwamo kuvinjari, kukumbatiana na pia kupigana mabusu, matukio ambayo yalizua ngumzo huenda walikuwa wakichumbiana.

Hata hivyo, baadaye walijitokeza na kuweka wazi kuwa hakukuwa masuala ya mahaba yalikuwa yakiendelea baina yao.

Cha kushangaza, walidai uhusiano wao ulikuwa wa kirafiki na kuegemea masuala ya kibiashara.

  • Tags

You can share this post!

Wamaua asikitishwa na tabia za wanaume kubaka watoto

Afisa wa polisi alazimika kutumia mitandao kuomba mke arejee

T L