• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
Jeraha kumkosesha kipa Ramsdale mechi mbili zijazo za Uingereza

Jeraha kumkosesha kipa Ramsdale mechi mbili zijazo za Uingereza

Na MASHIRIKA

KIPA wa Arsenal, Aaron Ramsdale, 23, atakosa mechi za kimataifa zitakazosakatwa na Uingereza katika kipindi cha wiki mbili zijazo baada ya kupata jeraha la paja.

Mlinda-lango huyo alikosa mechi ya Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) iliyoshuhudia waajiri wake Arsenal wakicharaza Aston Villa 1-0 mnamo Jumamosi na kukalia vizuri katika nafasi ya nne kwenye msimamo wa jedwali kwa alama 54.

Ramsdale alikuwa amejumuishwa katika kikosi cha wanasoka 25 walioitwa kambini na kocha wa Uingereza Gareth Southgate kwa ajili ya michuano miwili ijayo ya kirafiki dhidi ya Uswisi na Ivory Coast.

Kwa mujibu wa kocha Mikel Arteta wa Arsenal, jeraha la Ramsdale litamweka mkekani kwa “wiki chache zijazo”.

Mechi dhidi ya Villa ugani Villa Park mnamo Jumamosi ndiyo ya pekee kwa Ramsdale kutochezea Arsenal katika EPL tangu atwae nafasi ya kipa chaguo la kwanza, Bernd Leno mnamo Agosti baada ya waajiri wake kupokea kichapo kinono cha 5-0 kutoka kwa Manchester City.

Southgate tayari atakosa huduma za beki Trent Alexander-Arnold wa Liverpool ambaye anauguza jeraha la paja.

You can share this post!

Chelsea wapewa Real Madrid katika robo-fainali ya UEFA

AC Milan warejea kileleni mwa jedwali la Serie A

T L