FLORAH KOECH Na CHARLES WASONGA
SERIKALI imeshikilia kuwa kafyu iliyowekwa katika kaunti tatu zilizokumbwa na mapigano kaskazini mwa bonde la ufa haitaondolewa hadi usalama urejee maeneo hayo.
Kamishna wa Ukanda wa Bonde la Ufa Maalim Mohamed alisema kuwa visa vya wizi wa mifugo vingali vinashuhudiwa katika kaunti za Baringo, Elgeyo Marakwet na Pokot Magharibi hata baada ya serikali kutangaza kafyu kuanzia Juni 7.
“Kafyu itaendelea kwa sababu wakazi wamedinda kutia amri inayowataka kusalimisha silaha haramu. Wamekataa kutoa nafasi kwa mazungumzo na ndio maana tunaendelea kushuhudia vita,” akasema Bw Mohamed.