NA KALUME KAZUNGU
RAIS William Ruto amewasili katika kisiwa cha Kizingitini, Lamu Mashariki ambapo tayari amefungua rasmi chuo cha mafunzo anuwai cha Kizingitini TTI.
Pia ameongoza ufunguzi wa barabara ya kilomita 38 ya Kizingitini-Mtangawanda ambayo itakuwa ya lami.
Hii itakuwa mara ya kwanza kwa eneobunge la Lamu Mashariki kupata barabara ya lami.
Mbunge wa Lamu Mashariki ni Kapteni Ruweida Obo.
Soma Pia: Eneobunge lisilo na hata inchi moja ya lami tangu uhuru