• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 10:24 AM
Malindi Progressive yatamba ikifinyanga vipaji na kukuza maadili mema

Malindi Progressive yatamba ikifinyanga vipaji na kukuza maadili mema

Na PATRICK KILAVUKA

Malindi Progressive inapatikana Alaskan, Kaunti ndogo ya Kilifi.

Imekumbatiwa na jamii, japo nguzo ya uhimili inatoka kwa mfadhili Rashid Odhiambo kama njia ya kurudishia jamii mkono katika ukuzaji wa vipaji vya soka mashinani na kuwa kitovu cha kuondoa maovu ya kijamii, kukuza maadili mema, kuwapatia nafasi za kazi na kusaidia wale wanaosoma kwa kuwafadhili.

Kwa miaka tano sasa, timu ingali uhai ikiwa na wachezaji 30 mseto wa wanafunzi, vijana wa mtaani na wachezaji wengineo ambao wanasakata kabumbu katika Ligi ya Kitaifa Daraja ya Kwanza.

Imekuwa moto wa kuotea mbali kwani kufikia sasa, inashikilia nafasi ya pili na alama 17 ligini nyuma ya Dimba Patriots (18) kufikia kunakiliwa kwa makala haya. Kabla kukwea hadi Ligi ya Divisheni ya kwanza, ilikuwa imesimama imara kutoka Ligi ya FKF, Kaunti ndogo ya Kilifi, ya Kaunti ya Mombasa, Kanda ya Pwani, Ligi ya Kitaifa Daraja ya Pili kabla kutulia katika ya Daraja ya Kwanza Kitaifa.

Malindi Progressive (jezi ya bluu) ikicheza dhidi ya Kibera Soccer ugani NCC,Nairobi…Picha/PATRICK KILAVUKA

Ingawa hivyo, ilikuwa guu moja ndani ya Supaligi lakini ikang’atuliwa na Avena 3-0 ligi ya kutafuta atayefuzu “Main League”. Chini ya usukani wa wadau kocha Kassim Katana na msaidizi wake Billy Mwangemi, ndoto ya timu kushiriki Ligi ya Supa Kitaifa ingalipo.

Kuhakikisha wamevuka daraja kiligi, wamesajili kiungo John Owino, fowadi Athaman Aba, mawinga Daniel Atito na Julius Menza, mlinzi Daniel Makoli na mfumaji Isa Adima kusuka kikosi zaidi.

Wametoa mchezaji Samson Ndegwa ambaye alisajiliwa na Wazito FC kabla kurudi zizini. Hatimaye, wadau wanakiri kwamba, subira ndicho kigezo cha imani yao kuafikia ndoto ya kusonga mbele kidaraja.

Benchi ya kiufundi ya Malindi Progressive, Malindi,Kaunti ya Kilifi ikiongozwa na kocha Kassim Katana kwa pichani…Picha/PATRICK KILAVUKA

You can share this post!

Lewandowski abeba Bayern Munich dhidi ya Augsburg katika...

Ruto akaidi NCIC, atoa wimbo wa ‘Sipangwingwi’

T L