• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 6:50 AM
Mandago adai Gavana Bii alirithi Sh104 milioni za mpango wa elimu ng’ambo

Mandago adai Gavana Bii alirithi Sh104 milioni za mpango wa elimu ng’ambo

NA JARED NYATAYA

ALIYEKUWA Gavana wa Uasin Gishu na Seneta wa sasa wa kaunti hiyo Jackson Mandago ametofautiana na Gavana Jonathan Bii aliyedai Jumanne wiki hii kwamba alipata mfuko wa mpango wa kuwapeleka wanafunzi kujiunga na vyuo vikuu nchini Canada na Finland ukiwa na Sh1.8 milioni pekee.

Akihutubia wanahabari mjini Eldoret mnamo Ijumaa, Julai 14, 2023, Bw Mandago amedai kwamba alikabidhi mamlaka kwa Bw Bii almaarufu Koti Moja, akaunti ya mpango huo ikiwa na Sh104 milioni.

“Mrithi wangu alipata akaunti hiyo ikiwa na Sh104 milioni na wala sio Sh1.8 milioni alizosema,” amesema Bw Mandago.

Mpango huo unazingirwa na sakata kubwa kwa sababu wanafunzi wengi hawakujiunga na vyuo vikuu katika mataifa hayo ya kigeni jinsi walivyokuwa wameahidiwa.

  • Tags

You can share this post!

Maandamano ya Azimio kufanyika siku tatu kila wiki

Ruto asema hatakubali maandamano dhidi ya serikali ya KK

T L