• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 10:08 PM
Matiang’i aagiza machifu kusaka wanafunzi watakaokaidi kurudi shule

Matiang’i aagiza machifu kusaka wanafunzi watakaokaidi kurudi shule

Na George Odiwour

WAZIRI wa Usalama Dkt Fred Matiang’i ameagiza machifu kusaka watoto ambao watakosa kuripoti shule zitakapofunguliwa baada ya wiki mbili zijazo.

Waziri Matiang’i aliagiza makamishna wa kaunti, manaibu wao na machifu kuzuru shule zote kuanzia Januari 4, mwaka ujao ili kubaini idadi ya wanafunzi watakaokosa kuripoti.

Dkt Matiang’i aliyekuwa akizungumza alipojiunga na mke wa kiongozi wa ODM, Bi Ida Odinga, wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa maktaba katika Shule ya Upili ya Wasichana ya Ogande, Kaunti ya Homa Bay, aliwataka machifu kurekodi idadi ya wanafunzi watakaokuwa shuleni kila siku.

“Machifu wanafaa kuandaa mikutano ya kuhamasisha watu katika maeneo yao kuhusu umuhimu wa elimu,” akasema.

Miongoni mwa wanafunzi wanaomulikwa na serikali ni wasichana ambao walipata ujauzito wakati wa likizo ndefu iliyosababishwa na virusi vya corona. Kwa mfano, wasichana 7,200 walipata ujauzito kati ya Machi na Desemba, mwaka huu, kulingana na Waziri Matiang’i.

Kwa mfano, wasichana 7,200 walipata ujauzito kati ya Machi na Desemba, mwaka huu, kulingana na Waziri Matiang’i.’Machifu pamoja na wasaidizi wao wanastahili kushirikiana na maafisa wa elimu kuhakikisha kuwa watoto wote wanarejea shuleni. Serikali haitakubali kisingizio cha aina yoyote,” akaongezea.

Bi Odinga aliitaka serikali kuhakikisha pia kuwa watoto wa kiume wanarejea shuleni.Alisema watoto wengi wa kiume wanajihusisha katika biashara na kazi mbalimbali na huenda wakakataa kurejea shuleni.

“Watoto wengi wa kiume sasa wanajihusisha na biashara za bodaboda. Wengine wanafanya kazi ya mjengo. Serikali ihakikishe kuwa wavulana hao wanarejea shuleni,” akasema.

You can share this post!

Wakenya wasafiri mashambani licha ya onyo la serikali

CHARLES WASONGA: Matokeo ya Msambweni yasihusishwe na BBI...