• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 12:30 PM
MbS atarajiwa kutanzua mkwamo baina ya India na Pakistan

MbS atarajiwa kutanzua mkwamo baina ya India na Pakistan

Na AFP

KASHMIR, INDIA

MAJESHI ya India yalipata pigo Jumatatu katika vita ambavyo yanashiriki na wapiganaji wa Kashmir, baada ya tisa wao kuuawa.

Uvamizi huo unakuja siku chache baada ya shambulio jingine la muuaji wa kujitoa mhanga, wakati joto linazidi kupanda kati ya India na nchi jirani ya Pakistan.

Leo Jumatano Mwanamfalme wa Saudi Arabia Mohammed bin Salman, maarufu kama MbS inatarajiwa kwamba akiwa jijini New Delhi katika ziara yale ya kibiashara hasa, atazungumzia uhusiano baina ya India na Pakistan kujaribu kutanzua mkwamo uliopo.

India ililaumu Pakistan kwa shambulio hilo la Alhamisi wiki iliyopita dhidi ya msafara wa magari ya kijeshi, ambapo wanajeshi 14 waliangamia.

Katika vamizi hilo la Jumatatu, makabiliano makali ya bunduki yalichacha kwa zaidi ya saa nne katika wilaya ya Pulwama, kusini mwa Jiji kuu la Kashmir, Srinagar, wakati maafisa wa serikali walitangaza kuwa wanajeshi wanne, afisa wa polisi, wanamgambo watatu na raia mmoja waliuawa.

Kati ya waliouawa ni afisa wa kijeshi wa ngazi ya Meja. Aidha, wapiganaji watatu wa upande wa Jaish-e-Mohammed (JeM) wa Pakistan, kundi ambalo lilijigamba kutekeleza vamizi la wiki iliyopita, maafisa wa polisi na jeshi wakasema.

Maafisa sita wa ngazi za juu katika jeshi na polisi walijeruhiwa katika makabiliano ya bunduki yaliyofuata.

Mamia ya wanajeshi walivamia vijiji na kuvamia kwa risasi katika eneo lililoshukiwa kuwa maficho ya wanamgambo hao.

You can share this post!

Majimbo 16 yaishtaki serikali ya Trump

UKUMBI WA LUGHA NA FASIHI: Vipengele vikuu...

adminleo