• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Pete ya ukeni kinga ya maambukizi ya HIV, wasema watafiti

Pete ya ukeni kinga ya maambukizi ya HIV, wasema watafiti

Na Winnie Oyando

Matumizi ya pete ya ukeni (vaginal ring) miongoni mwa wanawake yanaweza kuzuia maambukizi ya virusi vya HIV, kulingana na watafiti kutoka Taasisi ya Dawa nchini (Kemri).

Wakiongozwa na mtafiti Beatrice Nyagol wa KEMRI, wanasema hatua hiyo ni njia ya kutatua utata wa matumizi ya tembe ya kila siku ya pre-exposure prophylaxis (PrEP) miongoni mwa walio katika hatari ya kuambukizwa virusi hivyo.

“Tunafanya majaribio ya kliniki kwenye pete ya ukeni ili kuwapunguzia mzigo wanawake walio katika hatari ya kuambukizwa virusi vya HIV, mzigo wa kumeza tembe za pre-exposure prophylaxis (PrEP),” akasema Bi Nyagol.

Pete hiyo imetengenezwa na ‘silicone’ na inyoingizwa ukeni, huwa na dawa ya ‘dapivirine’, inayoua virusi vya HIV ukeni.Pete hiyo hubadilishwa baada ya mwezi mmoja.

Bi Nyagol anasema pete hiyo imepita vipimo vyote na kupatikana kuwa salama kwa matumizi.“Kilichobaki ni kuiwasilisha kwa Bodi ya Dawa na Sumu ya Kenya ili iidhinishwe,” anasema Bi Nyagol.

Hivi sasa watafiti wametoa pete za uke kwa zaidi ya wanawake 4,500, pamoja na wajawazito na akina mama wanaonyonyesha, katika nchi za Uganda, Kenya, Zimbabwe, na Malawi.

 

You can share this post!

NYS sasa ni safi kama pamba, afisa mkuu asifia mageuzi

LEONARD ONYANGO: Siasa zimesaidia wafisadi kuendelea...