• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 2:56 PM
UCL: Bayern na PSG kukabana tena

UCL: Bayern na PSG kukabana tena

PARIS, Ufaransa

Huku wakikabiliwa na kibarua kigumu cha kubadilisha kichapo cha 3-2 kutoka kwa Paris Saint-Germain (PSG) katika pambano la Klabu Bingwa barani Ulaya, Bayern Munich watakuwa ugenini leo usiku kwa mechi ya marudiano ugani Parc des Princes jijini hapa.

Ushinidi wa ugenini ugani Allianz unawapa PSG matumaini ya kusonga mbele na kufuzu kwa nusu-fainali ya michuano hii ya thamani kubwa.

Mwishoni mwa wiki, vijana hao wa kocha Mauricio Pochettino waliandikisha ushindi mkubwa wa 4-1 dhidi ya Strasborg katika mechi ya Ligi Kuu ya Ufaransa (Ligue 1), wakati Bayern wakiweza tu kupata sare ya 1-1 dhidi ya Union Berlin.

Katika mkondo wa kwanza, Bayern walicheza bila mfungaji wao mkuu Robert Lewandowski, wakati PSG walinufaika pakubwa kupitia kwa Kylian Mbappe aliyefunga mabao mawili. Eric Maxim Coupo-Moting na Thomas Muller walifunga mabao ya Bayern simu hiyo.

PSG hawajawahi kushindwa nyumbani kwao na klabu ya Ujerumani, huenda wakaendeleza rekodi hiyo kwa kubandua mabingwa hao watetezi. Hata hivyo haitakuwa mteremko dhidi ya vijana wa Hansi Flick ambao wataingia uwanjani kuwania mabao ya mapema kwa lengo la kubadilisha mtokeo ya 3-2.

Bayern wameshindwa katika hatua hii mara moja tu katika misimu 10 iliyopita, waliposhindwa katika mkondo wa kwanza wa mechi za maondoano msimu wa 2014-15.

Kikosini, kocha Flick anajivunia wachezaji wa kila aina, wakiwemo Jamal Musiala na Marcus Ingvartsen.

Wataingia uwanjani wakati wakiendelea kufanya vizuri katika ligi kuu ya Bundesliga ambako wanaongoza kwa mwanya wa pointi tano mbele ya RB Leipzig.

You can share this post!

Sokomoko mpya Amerika raia mwingine mweusi akiuawa

Uozo wa kimaadili miongoni wa wabunge waanikwa