Vijana wakaidi wazee 2022

Vijana wakaidi wazee 2022

Na BENSON MATHEKA

SIASA za uchaguzi mkuu wa mwaka 2022 zinapoendelea kupamba moto, wazee wa jamii mbalimbali wamekuwa wakijitokeza kutoa misimamo yao inayotofautiana na vijana.

Wazee hao wamekuwa wakitawaza baadhi ya wagombeaji urais ambao vijana wanaonekana kutowachangamkia.

Wadadisi wa siasa wanasema kwamba hatua ya wazee hawa inaenda kinyume na misimamo ya vijana wanaohisi kwamba wana uhuru wa kuamua viongozi wanaowataka wawawakilishe.

“Kuna mgogoro wa uamuzi wa wazee wa baadhi ya jamii kutawaza wagombeaji na vijana wanaohisi kwamba wana uhuru wa kuchagua kiongozi wanayemtaka. Hii si kwa wanaogombea urais pekee bali hata wanaogombea viti vya ugavana, ubunge na useneta. Baadhi ya wazee wa jamii wanagawanya nyadhifa za uongozi kwa misingi ya ukoo jambo ambalo vijana hawafurahii,” asema Dkt Shadrack Ivuti, mtaalamu wa Masuala ya Jamii na Utawala.

Wazee wa Jamii ya Agikuyu wenyewe kwa wenyewe walitofautiana baadhi yao walipomtawaza Spika wa Bunge la Kitaifa Justin Muturi kuwa msemaji wa jamii ya Gema baadhi wakijitenga na hatua hiyo na hata kuandaa utakaso wa madhabahu ya jamii hiyo katika Kaunti ya Murang’a.

Kundi moja la wazee hao linasemekana kumchangamkia kiongozi wa chama cha ODM Raila Odinga na liliongoza ujumbe kumtembelea nyumbani kwake Bondo, Siaya ambapo lilikutana na wazee wa jamii ya Waluo.

Hatua ya wazee hao ilikuwa ya kuzika tofauti za kisiasa kati ya jamii hizi mbili kabla ya uchaguzi mkuu ujao mwaka 2022 na kumwidhinisha Bw Odinga kama mrithi wa Rais Uhuru Kenyatta.

You can share this post!

Mshukiwa wa tatu katika mauaji ya Tirop anyakwa

Uhuru adokeza kuwa huenda akaondoa kafyu

T L