Na SIAGO CECE,
WAHUDUMU katika fuo za bahari Kaunti ya Kwale wameanza kupewa chanjo ya kuepusha maambukizi ya virusi vya corona.
Mwenyekiti wa Chama cha Wanawake katika Utalii, tawi la Kwale, Bi Pauline Nduva, alisema hatua hiyo imenuiwa kuhakikishia watalii usalama wao dhidi ya Covid-19.
Chanjo hiyo imetolewa kwa ushirikiano na Idara ya Afya ya Kaunti ya Kwale., ambayo ilikubali kupeleka chanjo karibu na wahudumu katika fuo za bahari.