NA STEPHEN ODUOR
WAZAZI katika Kaunti ya Tana River, wametoa wito kwa Wizara ya Elimu kufutilia mbali likizo fupi za mihula.
Wakiongozwa na Bi Jane Simon, wazazi hao wamelalamika kuwa ni gharama kubwa kupeleka watoto shuleni hivi majuzi kisha wanarudi nyumbani baada ya muda mfupi.
Kulingana nao, watoto walikuwa na likizo ndefu ya miezi miwili kwa hivyo si busara kuwapa tena likizo fupi katikati ya muhula.