Dimba

Klabu yamgombeza kipa Trapp kwa kutumia nguvu zote kumkata kiu mpenziwe na kusahau taaluma

June 11th, 2024 1 min read

NA CHRIS ADUNGO

KLABU ya Eintracht Frankfurt ina wasiwasi kwamba kipa wake Kevin Trapp, 33, “anapotoshwa kitaaluma na kuvurugwa kiakili” na mchumba wake Izabel Goulart ambaye anapenda ngono kupindukia.

Trapp, ambaye ni golikipa wa Ujerumani, amekuwa katika uhusiano wa kimapenzi na mwanamitindo huyo maarufu raia wa Brazil tangu 2015 walipokutana akiwadakia Paris Saint-German (PSG).

Gazeti la Ujerumani la Bild limedai kuwa uhusiano wa wawili hao umegeuka kuwa mada ya kawaida ya katika mazungumzo ya wengi huko Frankfurt.
Klabu hiyo ya Bundesliga inaaminika kuwa na wasiwasi kwamba Trapp anatatizika kitaaluma kutokana na matakwa mengi ya kidosho wake “asiyeridhika chumbani upesi.”

Mojawapo ya mambo yaliyotajwa ni jinsi Trapp anaweza kutoka garini zaidi ya mara 50 kwa siku akisafiri na Izabel, 39, kwa ajili ya kumpiga picha kisura huyo.

Ripoti ya matukio inaonyesha kuwa uchezaji wa Trapp hata nyakati za mazoezi umeshuka pakubwa.

Izabel, 39, ni mwanamitindo maarufu ambaye aliwahi kufanya kazi nyingi za kuvumisha bidhaa na huduma za kampuni mbalimbali. Maisha yake ya kimapenzi na Trapp yamekuwa gumzo la mara kwa mara tangu kipa huyo kujipata katika ulazima wa kususia ngono kila mara timu yake inapopoteza mechi.

Izabel amewahi kudai kwamba yeye na Trapp hushiriki ngono mara nne au tano kwa wiki.

“Lakini kama amecheza katika mchezo muhimu na timu yake ikapoteza, ninaweza kujirembesha kabisa hadi nitengeneze kucha na kuvalia nguo fupi kabisa za kuvutia na bado hakutakuwa na ‘mchezo’ wowote katika chumba chetu cha kulala,” akasema.

Videge hao walianza kutoka pamoja kimapenzi mnamo 2018 ila bado hawajafunga pingu za maisha.