Afya na Jamii

Mafuriko: WHO yawataka Wakenya kuwa waangalifu kuepuka maambukizi

May 12th, 2024 1 min read

NA CHARLES WASONGA

Serikali, kupitia Wizara ya Afya, imeweka mpango wa kufuatilia mikurupuko ya magonjwa wakati wa msimu kama huu wa mvua za masika.

WHO pia imenunua karibu vifaa 87 vya kudhibiti kipindupindu na vifaa 20 vya kuzuia msambao wa ugonjwa wa nimonia na ambavyo vinasambazwa kwa kaunti zilizoathirika zaidi na mafuriko. Vifaa hivyo vinaweza kuwafaa karibu watu 10,000.

“WHO itaendelea kupiga jeki mikakati ya dharura ya kuzuia mikurupuko ya magonjwa ambayo yanaweza kuenea kwa haraka,” akasema Dkt Abdourahmane Diallo, ambaye ni mwakilishi wa WHO nchini Kenya.