Demu ashtuka kujua kalameni aliyeshuku ni mwizi aliomoka
MAKIMA, Embu:
POLO mmoja amezua gumzo mtaani hapa baada ya kusimulia jinsi kipusa aliyekuwa akimmezea mate alivyokataa kupanda gari lake akidai ni la kukodisha.
Mwanadada huyo aliamini kijana huyo hakuwa na uwezo wa kumiliki gari kwa sababu anatoka familia maskini.Jamaa alisema hakubishana naye wala kujitetea.
Badala yake, alimwacha aamini alichotaka.
Miezi kadhaa baadaye, demu alibaini kuwa gari hilo lilikuwa mali yake halali na alikuwa amejiendeleza kimya kimya kupitia biashara zake.
Baada ya ukweli kufichuka, msichana huyo alianza kutaka kufufua mawasiliano, lakini jamaa hakutaka uhusiano naye tena akidai alimdharau.
Kisa hicho kimezua mjadala mkubwa hapa, wengi wakisema si busara kumhukumu mtu kwa asili ya familia yake au mali anayoonekana kuwa nayo.