Blue Nile FC yaishinda maarifa Rhino FC

Bao la pili lilifumwa kimiani na mshambulizi matata Francis Kimani katika dakika ya 42.
Gongagonga
Kipindi cha lala salama vijana wa Blue Nile waligeuza msimamo wao wa ushambulizi huku wakizingatia gongagonga za chini chini ambapo straika wao Joseph Mburu alionyesha umahiri wake wa kusakata boli na kufunga mabao mawili mfululizo dakika ya 64 na 70.
Kocha wa Blue Nile anakiri ya kwamba vijana wake walipiga soka safi iliyowapa matumaini ya kusonga mbele kwenye jedwali la Ligi hiyo.
“Kwa sasa ninaongoza kwa alama tisa baada ya kuchapa mechi tano. Hata hivyo mechi ya hapo awali dhidi ya Ruiru Sports Academy tulilala mabao 2-0,” alisema kocha huyo.
Kwingineko, Mutomo FC ya Gatundu ililazimika kutoka sare ya 1-1 dhidi ya JYSA FC; nayo Maragua HomeBoyz ilitoka sare ya mabao 3-3 na Ruiru Sports Academy. Mechi hiyo ilipigiwa katika uwanja wa Ruiru.