• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 7:00 PM
Wanafunzi 400 wenye funza wanufaika

Wanafunzi 400 wenye funza wanufaika

Na FADHILI FREDRICK

WANAFUNZI 400 kutoka shule za msingi za Kilole na Zigira wamenufaika na mradi wa kupambana na funza uliozinduliwa na shirika la Ahadi Trust Kenya katika Kaunti ya Kwale.

Afisa Mkuu Mtendaji wa  shirika hilo, Dkt Stanley Kamau alisema vita dhidi ya funza ni muhimu ili kuwawezesha watoto kusoma katika mazingira mazuri bila usumbufu.

Akizungumza katika shule ya msingi ya Kilole wakati wa usambazaji wa dawa za funza, viatu na sodo kwa wanafunzi, Bw Kamau alisema Kwale ni kati ya kaunti zitakazonufaika kwa Sh2 milioni za kupambana na funza.

“Tumeweka Sh2 milioni kwa kila kaunti ili kupambana na funza  ili kuruhusu watoto wetu kusoma katika mazingira mazuri na kuwawezesha kufanya vizuri katika masomo yao,” alisema.

Bw Kamau alitumia fursa hiyo kuwashawishi wazazi kubuni miradi ambayo itawasaidia kupigana na umaskini na kuboresha viwango vyao vya maisha.

Hata hivyo, aliongeza kwamba mwezi Machi mwaka huu, shirika hilo litafanya utafiti wa kina nchini ili kubainisha ni maeneo yapi ambayo yana katika hatari kuu ya funza kuwaathiri wakazi.

Alisema utafiti huo utatoa ripoti kamili ambayo italisaidia shirika hilo kupambana na mdudu huyo hatari.

 

You can share this post!

Atwoli ataka Duale apokonywe kazi

Dhamira kuu ya Miguna Miguna yaonekana ni kujitakasa apate...

adminleo