• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 9:50 AM
Ufaransa yaahidi kusaidia Iraq kujijenga upya

Ufaransa yaahidi kusaidia Iraq kujijenga upya

Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Ufaransa Jean-Yves Le Drian. Picha/ Hisani

Na MASHIRIKA

WAZIRI wa Mashauri ya Kigeni wa Ufaransa Jean-Yves Le Drian Jumatatu aliizuru Iraq ili kuangazia mikakati ya ujenzi mpya wa taifa hilo baada ya kukumbwa na mapigano kwa muda mrefu.

Hayo yanajiri baada ya serikali ya Iraq kutangaza kulishinda kundi la kigaidi la Islamic State (IS) ambalo limekuwa likiisumbua katika sehemu mbalimbali nchini humo.

“Nimekuja ili kueleza kujitolea kwa Ufaransa katika juhudi safari ya kuijenga mpya (Iraq). Daima tutakuwa pamoja nanyi. Tumekuwa hapa katika harakati za kuleta amani, na tukakuwepo mnapoanza kurejesha uthabiti wa nchi,” akasema Bw Le Drian.

Ufaransa ilikuwa mojawapo ya nchi ambazo zilishirikiana na Iraq kwenye operesheni yake dhidi ya kundi la IS, baada ya kundi hilo kuteka maeneo mengi ya mpaka kati yake na Syria mnamo 2014.

Kwa sasa, Iraq inatafuta wahisani kuisaidia kuijenga upya, kutokana na uharibifu mkubwa ambao ulisababishwa na mapigano hayo.

Aidha, mikakati hiyo ni pamoja na maandalizi ya kongamano la kuchanga fedha katika nchi jirani ya Kuwait, ambalo lilianza Jumatatu.

 

You can share this post!

Jeshi la Misri lasema limeua magaidi 12 katika operesheni

Kamari yageuka janga kuu nchini

adminleo