• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 1:14 PM
Kituo cha redio cha Kikristo chafungwa kudunisha wake

Kituo cha redio cha Kikristo chafungwa kudunisha wake

Na AFP

KIGALI, RWANDA

SERIKALI Jumatatu ilifunga kituo cha redio cha Kikristo kwa kupeperusha mahubiri ya kuwadunisha wanawake.

Kituo cha Amazing Grace FM, kinachomilikiwa na Amerika, kilifungwa kwa miezi mitatu baada ya mhubiri wake Nicolas Niyibikora kuwataja wanawake kama hatari, waovu na wavunjaji wa mipango ya Mungu mnamo Januari 29.

Mahubiri hayo yalishutumiwa na makundi mbalimbali ya wanaharakati. Chama cha Wanahabari Wanawake nchini Rwanda kiliripoti kituo hicho kwa Tume ya Kusimamia Vyombo vya habari.

Tume pia imemtaka mhubiri huyo kuomba msamaha kwa kutoa matamshi ya kuwadunisha wanawake katika mahubiri yake.

 

  • Tags

You can share this post!

ANC sasa yamkabidhi Rais Zuma barua rasmi ya kumtaka...

Msemaji wa Machar kunyongwa kwa kujaribu kupindua serikali...

adminleo