• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 3:03 PM
Utafiti: Wasiotafuna mlo vyema hatarini kunenepa kupindukia

Utafiti: Wasiotafuna mlo vyema hatarini kunenepa kupindukia

Na MASHIRIKA

WATU wanaofakamia chakula bila kutafuna wako katika hatari ya kuwa wanene kupindukia, kulingana na matokeo ya utafiti uliotolewa Jumanne.

Utafiti huo uliofanywa na Chuo Kikuu cha Kyushu na kuhusisha watu 60,000 nchini Japan, ulibaini kuwa watu wanaokula polepole na kutafuna chakula kwa muda mrefu wana nafasi finyu ya kuwa wanene kupindukia ikilinganishwa na wale wanaokula harakahara.

Watafiti walichunguza na kufuatilia kwa karibu tabia za watu walioshiriki utafiti huo kati ya 2008 na 2013

Idadi kubwa ya watu 4,192 wanaokula polepole na kutafuna chakula kwa muda mrefu, walipatikana na uzito wa chini.

Idadi kubwa ya watu walikula kwa kasi bila kutafuna walipatikana wakiwa na uzito kupindukia.

Watafiti walibaini kuwa watu wanene waliobadili tabia na kuanza kutafuna chakula kwa muda mrefu, ndani ya kipindi cha miaka sita, walipunguza uzito kwa kiasi kikubwa.

Watafiti pia waligundua kuwa watu wanaokula kila mara wako katika hatari ya kuwa wanene kupindukia.

 

  • Tags

You can share this post!

Msemaji wa Machar kunyongwa kwa kujaribu kupindua serikali...

FATAKI: Si lazima kuzaa au kuolewa ndipo ukamilike kama...

adminleo