• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 5:23 PM
Taharuki yatanda kijijini mwanamume kuvamiwa na kuuawa kanisani

Taharuki yatanda kijijini mwanamume kuvamiwa na kuuawa kanisani

Na MAGDALENE WANJA

HOFU ilitanda katika kijiji cha Kimangu eneo la Rongai, kaunti ya Nakuru baada ya manamume mwenye umri wa miaka 75 kufariki baada ya kuvamiwa kanisani.

Bw Francis Imili alitoka nyumbani kwake na kuelekea kanisa la Sacred Heart Catholic Church Kimangu ambako amehudumu kama mwelekezi kwa zaidi ya miaka 20.

Ibada ilipokuwa ikiendelea, mwamume mwenye umri wa makamu aliingia kanisani huku akibeba fimbo na kumshambulia Bw Imili na kumgonga kichwani. Bi Peninah Wanjiru alisema kuwa alipogongwa kichwani na fimbo hiyo aliangukia kiti ambapo aliumiazaidi baada ya kugongwa usoni.

“Kabla ya kumkimbiza hospitalini, tulitumia vitambaa kufunga sehemu ya kichwa chake iliyokuwa ikivuja damu sana,” alisema Bi Wanjiru.

Hali ya Bw Imili iliendelea kuwa mbaya zaidi, alisema Bi Wanjiru, na wakalazimika kumpeleka katika hospitali ya Nakuru Level Five ambako alifariki akipokea matibabu.

Mkewe marehemu, Bi Tabitha Haluba, alisema kuwa mumewe alimuacha nyumbani kuelekea kanisani ila hakuandamana naye sababu alikuwa ametembelewa na wajukuu wake.

Bi Haluba alisema kuwa mumewe amemuacha na watoto 10 huku akiongeza kuwa baadhi yao bado wako katika shule ya upili.
Washirika wa kanisa hiyo, waliitaka serikali kuwapa ulinzi wanapohudhuria ibada

You can share this post!

Uzani mdogo wafanya vijana kukataliwa jeshi

Githu Muigai ainua mikono, Kihara na Ogeto ndani

adminleo