• Nairobi
  • Last Updated April 16th, 2024 10:55 AM
Mama ashinda mashindano bila kumpa fahali wake bangi

Mama ashinda mashindano bila kumpa fahali wake bangi

Na FAUSTINE NGILA 

Mama Peninah Otuma kutoka kijiji cha Ematetye amefunguka kuhusu vita vya ng’ombe akisema yeye hampi fahali wake chochote kabla ya mashindano.

Akifurahia ng’ombe wake kushinda vita vya ng’ombe katika Shule ya Upili ya Mwangaza katika kaunti ya Kakamega, Bi Otuma anasema kwamba yeye humlisha ng’ombe wake chakula cha kawaida tu kama nyasi na wala si jinsi baadhi ya washindanaji wanavyowapa ng’ombe wao bangi kuwafanya wawe na hasira kali ya kupigana.

Anaongeza kwamba yeye humuombea ng’ombe wake na kumuongelesha kabla ya vita hivyo. Bali na vita vya fahali, mashindano ya kila mwaka ya Toto Cup Cleophas Shimanyula yalijumuisha fani zingine kama kuvutana kwa kamba, soka ya wanaume, soka ya wanawake, voliboli ya wanawake, mpira wa pete na uendeshaji wa baiskeli.

Makala ya mwaka 2018 yalihudhuriwa na Seneta wa Kakamega Cleophas Malala na Mbunge wa Lurambi, Titus Khamala, miongoni mwa viongozi wengine wa eneo la Lurambi.

You can share this post!

Kosgei na Obiri wang’aa mbio za San Silvestre,...

2019: Ukosefu wa usiri wa data mitandaoni utazidi kuwaumiza...

adminleo