Shangazi Akujibu
SHANGAZI AKUJIBU: Nipe mbinu za kuongeza ladha chumbani
Wanandoa wakipiga gumzo kuhusu masuala ya fedha. Picha|Maktaba.
SWALI: Nilisoma ushauri wako hapa ukisema mapenzi hukosa ladha kama wahusika hawana ujuzi wa kuchochea hisia. Tafadhali nielezee jinsi ya kuchochea mambo chumbani ili kumridhisha mwenzangu.
Jibu: Njia za kuamsha hisia za kimapenzi ni nyingi. Unaweza kumsisimua mwenzako kutokana na jinsi unavyomtazama, kumzungumzia ama kumpapasa mwilini. Hizi ni baadhi tu za mbinu. Lakini kufaulu kwake hutegemea ubunifu wa mtu binafsi.
IMETAYARISHWA NA WINNIE ONYANDO