Shangazi Akujibu
SHANGAZI AKUJIBU: Mke wa bosi amenipenda, nahofia kufutwa!
Mteja akitumia simu ya mkono. PICHA|PEXELS
SWALI: Kwako Shangazi. Jana tulikuwa na kikao cha wafanyakazi kuboresha mahusiano ya kikazi (team-building) na tukaanza kuzungumza na mke wa bosi wangu. Baadaye akanitafuta kwenye WhatsApp akisema alifurahia mazungumzo yetu. Ninahofia Bosi akijua atanifuta kazi! Naomba ushauri wako.
Jibu: Usijichimbie kaburi. Mjibu kwa heshima na uweke mipaka. Ukicheza na moto, ofisi itakuwa jivu.
IMETAYARISHWA NA WINNIE ONYANDO