Shangazi Akujibu

SHANGAZI AKUJIBU: Kila kitu kwa mpenzi ni ‘ex’ wangu hivi, ‘ex’ vile!

Na SHANGAZI November 23rd, 2025 Kusoma ni dakika: 1

SWALI: Shikamoo Shangazi. Kila tukizungumza na mpenzi wangu, lazima ataje ex wake. Nimechoka kusikia habari kuhusu huyo mtu. Naona kama bado wanapendana.

Jibu: Mtu akimtaja ex mara kwa mara anaonyesha hajamsahau. Usigombanie nafasi ya pili. Chukua viatu vyako ukimbie.

IMETAYARISHWA NA WINNIE ONYANDO