Shangazi Akujibu
SHANGAZI AKUJIBU: Baba yangu yuko hai ila kamwe hataki tukutane, ninaumia sana moyoni
Baba akimgombeza mwanawe. Picha|Maktaba
SWALI: Shikamoo Shangazi. Nimegundua baba yangu yuko hai lakini hataki tukutane. Alinidanganya atanitafuta ila sijaona hadi leo. Naumia sana. Nifanye nini?
Jibu: Kukubaliwa na mzazi ni baraka, lakini kukataliwa si mwisho wa maisha. Mpe muda. Usilazimishe.
IMETAYARISHWA NA WINNIE ONYANDO