• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 5:50 AM
NYS yapewa ekari 100,000 kukuza pamba Galana-Kulalu

NYS yapewa ekari 100,000 kukuza pamba Galana-Kulalu

Wakulima wakivuna pamba katika eneo la Molo, Nakuru. Picha/ Maktaba

Na BERNARDINE MUTANU

HUDUMA ya Kitaifa ya Vijana (NYS) imepewa ekari 100,000 za mradi wa unyunyiziaji wa Galana-Kulalu.

Hii ni katika juhudi za serikali za kuzindua tena kilimo cha pamba. Rais Uhuru Kenyatta Ijumaa alisema mradi wa Galana-Kulalu uliambatana na ajenda nne za Jubilee.

Alisema hayo eneo la Gilgil wakati wa kuhitimu kwa vijana wa NYS. Katika mpango huo kilimo cha pamba kinatarajiwa kubuni nafasi 50,000 za kazi na ukuzaji wa mapato kutokana na mauzo ya nguo katika soko la kimataifa hadi Sh20 bilioni.

“Kama sehemu ya kuzindua tena sekta ya pamba, NYS itapewa ekari 100,000 za Galana-Kulalu,”alisema rais Ijumaa.

Mradi wa unyunyiziaji wa Galana-Kulalu ulilenga kuimarisha chakula nchini wakati ukame na njaa unaangamiza wananchi wengi.

You can share this post!

Mkaguzi mkuu sasa yuko huru kukagua hesabu za KDF

IEBC yasema inahitaji Sh8 bilioni kutathmini upya mipaka

adminleo