• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 1:29 PM
KAPI yataka teknolojia itumike kuzima biashara ya dawa feki

KAPI yataka teknolojia itumike kuzima biashara ya dawa feki

Mhudumu wa duka la dawa akitia tembe za dawa kwa chupa. KAPI imeonya kuwa huenda baadhi ya dawa zinazosafirishwa nchini zikawa feki. Picha/ Maktaba

Na BERNARDINE MUTANU

Chama cha Wauzaji Dawa nhini (KAPI) kimeitaka Bodi ya Dawa na Sumu nchini (KPPB) kuanza kutumia teknolojia ya dijitali kukomesha biashara ya dawa ghushi nchini.

Katika taarifa, KAPI ilisema bodi hiyo inahitaji kufuata meli za shehena zenye kubeba dawa ili kutambulisha bidhaa ghushi na kuzizuaia kuingia nchini Kenya.

“Bidhaa ambazo hazijaidhinishwa katika soko la humu nchini ni hatari zaidi kwa sababu huenda zilihifadhiwa vibaya ndani ya meli,” alisema mwenyekiti wa KAPI Bi Anastasia Nyalita katika taarifa hiyo.

Kulingana naye, bidhaa hizo bandia hubandikwa majina kwa lugha zingine ambazo ni vigumu kwa Wakenya kuelewa, kama vile Kituruki, Kiarabu na Kijerumani.

Chama hicho kilipongeza KPPB kwa kuchukua hatua kabambe kumaliza wauzaji wa dawa bandia nchini.

You can share this post!

Mawakili maarufu wateuliwa kupunguza mrundiko wa kesi...

Kipsang’ alenga tena kuvunja rekodi ya dunia kwenye...

adminleo