Na MARY WANGARI
LUGHA mwiko
Hii ni aina ya lugha ambayo matumizi yake yamefungiwa katika vigezo fulani vya utamaduni. Lugha mwiko pia inasheheni msamiati mahsusi ambao hauruhusiwi kutumiwa kiholela katika jamii. Mifano ni kama vile:
Msamiati huu huhusisha maneno ambayo hutamkwa katika mazingira fulani maalumu pekee. Madhumuni ya lugha mwiko katika jamii ni pamoja na:
Lingua franka (Lingua franca)
Lugha hii hutumiwa na watu walio na lugha tofauti kwa ajili ya mawasiliano. Mfano mzuri ni Kiswahili ambayo ni lingua franka katika eneo la Afrika Mashariki.
Sifa za Lingua Franka ni kama zifuatazo:
Lugha za taifa
Hizi ni lugha za asili za kikabila zinazozungumzwa katika nchi fulani mathalan baadhi ya lugha zinazozungumzwa nchini Kenya ni kama vile: Kikikuyu, Kiluhya, Kikamba nchini Kenya.
Nchini Tanzania kuna lugha kama vile: Kihaya, Kisukuma, Kibondei.
Pijini (Pidgin)
Hii ni lugha inayobuniwa na kutumiwa kwa mawasiliano baina ya watu ambao lugha zao ni tofauti na hawana lugha moja wanayoielewa kwa pamoja.
Sifa za pijini ni kama zifuatazo:
Marejeo
Chiraghdin, S., Mnyampala, M. (1977). Historia ya Kiswahili. Nairobi: Oxford University Press.
Richards, J.C. (1984). Error Analysis Perspectives on Second Language Acquisition. London: Longman Group Ltd.
Wardhaugh, R. (1986). An Introduction to Socio-Linguistics. New York: Blackwell Publishers.