• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 10:55 AM
UKUMBI WA LUGHA NA FASIHI: Matumizi ya vihisishi katika sajili isiyo rasmi

UKUMBI WA LUGHA NA FASIHI: Matumizi ya vihisishi katika sajili isiyo rasmi

Na MARY WANGARI

AGHALABU mazungumzo ya kawaida huandamana na matumizi ya vihisishi kama vile eeh! mmh! aah!

Vihisishi vilivyozoeleka katika Kiswahili ni masalale! na ala!

Hali hii hutokea ili kumpa msemaji fursa ya kufikiri na kuwa na uhakika na anachotaka kusema.

Ubadilishanaji au uchanganyaji ndimi

Ubadilishaji msimbo hutokea wakati ambapo mzungumzaji anasema katika lugha moja kisha baada ya muda akaongea kwa lugha ya pili na kuweza kuongea kwa muda.

Hali hii hutokea wakati ambapo wahusika katika mazungumzo wanapokuwa na uwezo wa kutumia lugha wanazozijua.

Aidha, ubadilishaji ndimi huweza kasababishwa na hali ya wahusika kuonyesha madaha hasa yanayochukuana na tabaka fulani.

Matumizi ya lugha rasmi, isiyo rasmi au lugha ya ucheshi na utani

Matumizi ya lugha kwa njia hii hutegemea wahusika na muktadha. Kwa mfano, mtoto anapoongea na baba yake katika hali ya kawaida, mara nyingi watatumia lugha rasmi kuonyesha heshima na unyenyekevu. Hiki ni kinyume na watani wawili ambao watatumia lugha ya utani na yenye ucheshi mwingi.

Msamiati kubadilikabadilika

Msamiati hubadilika kutegemea mada, uwezo wa lugha wa wasemaji na pia muktadha wa mazungumzo.

Iwapo wasemaji hawana umilisi mkubwa wa lugha, msamiati sahili unaoeleweka kwa urahisi utatumika.

Iwapo wana umilisi mkubwa, mazungumzo yatakolezwa kwa matumizi ya msamiati usiowa kawaida, pamoja na istilahi hasa kutegemea mada.

Sajili za lugha ni miundo au namna mbalimbali za matumizi ya lugha husika. Kila sajili au rejista ina sifa bainifu zinazoitofautisha na lugha jinsi ifuatavyo.

Sarufi – Vipengele vya kisarufi hujitokeza katika sajili kutegemea shughuli. Kwa mfano katika muktadha wa mahakamani na hospitalini, lugha itakuwa na miundomsingi ya kuamuru, kukanusha na maswali.

Kanuni za lugha – Kanuni zinazotawala matumizi tofauti kutegemea sajili. Kwa mfano, lugha ya kitaaluma huhitaji maneno yatamkwe kikamilifu na kwa usahihi.

Adabu: Lugha kwa mfano katika shughuli rasmi maabadini huwa yenye adabu, tofauti na lugha ya faraghani. Katika shughuli kama vile za tohara na ulevi, matumizi ya lugha chafu huwa jambo la kawaida.

 

[email protected]

Marejeo

Massamba, D.P.B., (2002). Historia ya Kiswahili 50 BK. Nairobi: Jomo Kenyatta Foundation.

Ipara, I. O. &  Waititu, F.G. (2006). Ijaribu na Uikarabati. Nairobi: Oxford University Press.

Habwe, J., (2006). Darubini ya Kiswahili. Nairobi: Phoenix Publishers.

Maddo, U. & Thiong’o, D. (2006). Mazoezi na Udurusu: Kiswahili 102/2. Nairobi: Global Publisher.

You can share this post!

Real Madrid, Bayern na Man U sasa zamezea mate Salah

Jamii za Mlima Kenya zinakosa nguvu za kiume kwa kuabudu...

adminleo