• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 12:48 PM
UKUMBI WA LUGHA NA FASIHI: Motisha katika kusoma na kufundisha lugha mpya

UKUMBI WA LUGHA NA FASIHI: Motisha katika kusoma na kufundisha lugha mpya

Na MARY WANGARI

MOTISHA au ari inaweza kufafanuliwa kama tabia au msukumo katika kutimiza malengo fulani.

Kwa mujibu wa TUKI (2004), motisha inaelezwa kwamba ni kitu kama vile fedha inayotolewa ili kumtia mtu hamasa kujifunza jambo.

Hata hivyo, si lazima umpe mtu kitu bali unamtia moyo mwanafunzi na kumsaidia. Mwalimu anapaswa kutumia motisha chanya na wala sio motisha hasi. Kwa mfano hutakiwi kuchapa fimbo

Kwa mujibu wa Brown (1994), anafafanua motisha kama:

i. Kiwango cha uchaguzi ambacho unafanya kuhusu lengo unalotaka kufikia

ii. Jitihada atumiazo mtu kufikia malengo hayo

Kwa upande wao Skinner4 & Wattson wanaangazia zawadi na uhimizaji kwa wanafunzi pamoja na adhabu ili kufifisha na kujenga hali fulani.

Kuna aina mbalimbali za motisha jinsi tutakavyoziainisha ifuatavyo:

i. Mwamko au ari ya mwanagenzi binafsi

ii. Mazingira mazuri ya kufundishia Kiswahili kwa mfano, darasa, nje na kadhalika

iii. Jamii inayomzunguka ni motisha pia

iv. Mwalimu anaweza kuwa motisha kwa mwanafunzi

v. Zana au vifaa vya kujifunzia pia ni motisha

 

Je, umeipenda mada hii? Tuandikie maoni au wasiliana na mwandishi: [email protected]

Marejeo

Chiraghdin, S. & Mnyampala, M. (1977). Historia ya Kiswahili. Nairobi: Oxford University Press.

Richards, J.C. (1984). Error Analysis Perspectives on Second Language Acquisition. London: Longman Group Ltd.

Wardhaugh, R. (1986). An Introduction to Socio-Linguistics. New York: Blackwell Publishers.

You can share this post!

UKUMBI WA LUGHA NA FASIHI: Sifa za mkufunzi, mwanagenzi...

UKUMBI WA LUGHA NA FASIHI: Dhana ya motisha ikiwemo matawi...

adminleo