• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 9:15 PM
AFCON: Mastaa watakaokosekana uwanjani na sababu zao

AFCON: Mastaa watakaokosekana uwanjani na sababu zao

Na GEOFFREY ANENE

KAMA wewe ni shabiki wa Pierre-Emerick Aubameyang, Joel Matip, Emmanuel Adebayor na Gervinho jua kwamba utahitajika kutafuta mchezaji mwingine wa kushabikia kwenye Kombe la Afrika (AFCON) kwa sababu wako katika orodha ya wachezaji nyota ambao pia watakuwa mashabiki nchini Misri kutoka Juni 21 hadi Julai 19, 2019.

Mshambuliaji wa Arsenal, Aubameyang, ambaye aliibuka mfungaji bora kwenye Ligi Kuu ya Uingereza msimu 2018-2019 kwa mabao 22 kwa pamoja na nyota wa Liverpool Mohamed Salah na Sadio Mane, hakuweza kusaidia Gabon kujikatia tiketi ya kuwa nchini Misri.

Gabon ilikuwa kundi moja na Mali na Burundi zilizonyakua tiketi, na Sudan Kusini.

Matip, ambaye alichezea Indomitable Lions ya Cameroon mara moja pekee tangu mwaka 2014, aliendelea kukataa mwito hata baada ya tetesi kwamba alitumiwa ujumbe kumuomba abadili msimamoa wake wa kutaka kuchezea klabu yake ya Liverpool pekee.

Gervinho aling’ara akiwa Arsenal miaka iliyoenda. Pia, aling’aa akichezea Parma kwenye Ligi Kuu ya Italia msimu 2018-2019 hata kutiwa katika kikosi cha Ivory Coast.

Hata hivyo, alitemwa dakika ya mwisho pale kocha Ibrahim Kamara alipoamua pengine muda wake katika timu ya taifa umeisha kwa kumuacha nje ya kikosi chake cha mwisho cha wachezaji 23.

Hii hapa orodha ya baadhi ya wachezaji nyota ambao watakosekana katika AFCON 2019:

Vincent Aboubakar (Cameroon) – mkekani akiuguza jeraha

Pierre-Emerick Aubameyang (Gabon) – Gabon haikufuzu

Gervinho (Ivory Coast) – alitemwa

Kelechi Iheanacho (Nigeria) – alitemwa

Juma Balinya (mfungaji bora Ligi Kuu Uganda) – alitemwa

Allan Wanga (Kenya) – alitemwa

Joel Matip (Cameroon) – alikataa mwito

Eric Bailly (Ivory Coast) – jeraha

Emmanuel Adebayor (Togo) – Togo haikufuzu

Aristide Bance (Burkina Faso) – Burkina Faso haikufuzu

Itumeleng Khune (Afrika Kusini) – jeraha

Jeffrey Schlupp (Ghana) – jeraha

Fashion Sakala (Zambia) – Zambia haikufuzu

Jacques Tuyisenge & Meddie Kagere (Rwanda) – Rwanda haikufuzu

You can share this post!

AFCON: Mamilioni yatakayong’ang’aniwa na timu 24

Amekuwa jela miaka 28 baada ya mwanamke kuota kuwa alimbaka

adminleo