• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 5:46 PM
MAPISHI: Jinsi ya kupika nyama yenye viungo mbalimbali na mboga

MAPISHI: Jinsi ya kupika nyama yenye viungo mbalimbali na mboga

Na MARGARET MAINA

[email protected]

Muda wa kuandaa: Dakika 10

Muda wa mapishi: Dakika 40

Walaji: 2

Vinavyohitajika

  • Nyama nusu kilo
  • Tangawizi ya unga kijiko 1
  • Mafuta ya kupikia
  • Kitunguu maji 1,
  • Juisi ya Limau
  • Kitunguu saumu punje 5
  • Pilipili mboga 2 za rangi tofauti
  • Chumvi kijiko 1
  • Pilipili

Maelekezo

Andaa nyama kwa kuikata vipandevipande ili viive vizuri na kwa urahisi. Osha na kisha weka kando.

Paka chumvi katika pande zote za nyama. Nyunyizia limau, tangawizi, na kitunguu saumu kilichopondwa. Hakikisha umepaka vizuri katika pande zote na kuenea vizuri. Weka pilipili kisha acha nyama ikae pembeni iingie viungo kwa muda wa robo saa.

Bandika kikaangio mekoni na uache kipate moto kiasi. Weka nyama ila usiweke mafuta. Acha vipande vya nyama viive taratibu huku ukiwa unageuza hadi nyama iwe rangi ya kahawia pande zote.

Kama nyama haijaiva na inakauka, nyunyizia maji kiasi ili ipate kulainika vizuri na kuiva kabla ya kuila.

Osha kisha kata pilipili mboga, kitunguu saumu, kitunguu maji na pilipili za kawaida. Hifadhi kwenye chombo safi.

Nyama ikishaiva vizuri, weka mafuta ya kupikia kiasi cha vijiko viwili kisha acha yapate moto kabla ya kutumbukiza hapo kitunguu maji. Koroga.

Funika kiasi ili vitunguu viive na kuwa na rangi ya kahawia.

Weka mboga mboga huku ukikoroga kila wakati kisha funika.

Acha mboga iive kwa mvuke kwa dakika tano. Bandua mboga,

Pakua na chochote ukipendacho na ufurahie mlo wako.

You can share this post!

Muda maalum wa sensa wakaribia kutamatika baadhi wakihofia...

Madereva 25 tayari kuonyeshana ubabe KCB Nanyuki Rally

adminleo