• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 2:16 PM
MAPISHI: Jinsi ya kuandaa wali wa nazi na nyama ya kusaga

MAPISHI: Jinsi ya kuandaa wali wa nazi na nyama ya kusaga

Na MARGARET MAINA

[email protected]

Muda wa kuandaa: Dakika 10

Muda wa kupika: Dakika 30

Walaji: 4

Vinavyohitajika kwa wali

  • Mchele kilo ½
  • Tui la nazi kikombe 1
  • Maji lita
  • Chumvi kijiko ½

Maelekezo

Osha mchele.

Weka mchele kwenye sufuria na ongeza chumvi. Acha mchele hadi uanze kuchemka katika sufuria mekoni.

Ukishaanza kuchemka, ongeza tui la nazi. Usikoroge.

Acha mchanganyiko uive taratibu kwa dakika 10.

Punguza moto na uache mchele uive hadi maji yakauke.

Epua.

Vinavyohitajika kwa nyama ya kusaga

  • Nyama ya kusaga kilo 1
  • Vitunguu maji 2
  • Vitunguu saumu 2
  • Tangawizi 1
  • Nyanya 4
  • Mafuta ya kupikia
  • Chumvi kijiko 1
  • Karoti 2
  • Pilipili mboga 1
  • Juisi ya limau

Maelekezo

Menya vitunguu, karoti, pilipili mboga na ukate hadi kuwa vipande vyembamba sana.

Menya nyanya na tangawizi kisha ukate vipande vipande.

Twanga vitunguu saumu kisha bandika sufuria ya kupikia mekoni.

Weka nyama na anza kukoroga ili kuzuia isigandie kwenye sufuria na kuungua.

Weka kitunguu maji huku ukiendelea kukoroga kwa muda wa dakika 10. Ongeza kitunguu saumu na tangawiizi huku ukikoroga.

Weka au mimina mafuta ya kupikia kisha weka pilipili mboga, karoti na juisi ya limau. Ongeza chumvi kidogo. Endelea kukoroga.

Weka nyanya, koroga na funika sufuria uache kwa dakika 10.

Pakua na wali wa nazi na ufurahie.

You can share this post!

SHANGAZI AKUJIBU: Tuliyeachana kisha tukarudiana hataki...

56 wafa katika mkanyagano Qasem Soleimani akizikwa

adminleo